Tuesday, 25 October 2011

Simba, Yanga nani zaidi Jumamosi?

Kocha wa Simba, Moses Basena
YANGA na Simba zinaingia kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam Jumamosi Oktoba 29, katika mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom, mchezo unaotarajiwa kuwa na upinzani.

Hata hivyo, tayari mashabiki wa Yanga wameanza 'minong'ono' hasa baada ya kocha wa sasa Sam Timbe kuondolewa na kuja kwa Kosta Papic kunaweza kuwavuruga wachezaji hasa kutokana na kila mmoja kuwa na mfumo wake wa uchezaji.

Simba vs Yanga
Mashabiki wa soka wanasema kuwa hiyo ni nafasi kwa Simba kutumia mwanya huo, lakini vilevile wapo wenye mtazamo tofauti wanaosema kuwa Simba wanaweza wakapigwa endapo watafikiria hayo na Yanga kutumia staili walioyoizoea ya Timbe.

Pamoja na hayo, Yanga ina kikosi ambacho zaidi wanamtegemea Kenneth Asamoah na Hamis Kiiza lakini kwa upande wa Simba, vilevile watakuwa na Haruna Moshi 'Boban', Emmanuel Okwi na Felix Sunzu. Boban na Sunzu ndiyo walioiua Yanga katika Ngao ya Jamii ya ufunguzi wa Ligi Kuu.


Kocha wa Simba, Moses Basena amekwishasema kuwa hana wasiwasi na Yanga kwa kuwa anachukulia kama mechi nyingine ya ligi.

Wakenya wahofia gharama za maisha kupanda

WAKATI majeshi ya Kenya yakielekea mpakani mwa Kenya na Somalia, tayari wananchi wa Kenya wameanza kuingiwa na wasiwasi wa kupanda kwa gharama za maisha kwamba kazi sasa itakuwa kuendeleza fedha kwa mapambano dhidi ya Al-Shabaab.
Itamlazimu mfanyakazi kulipa Sh7,000 na Sh10,000 (kati ya dola 70 hadi 100) kila siku kwa ajili ya kumwezesha askari mmoja kuishi katika uwanja wa mapambano; hiyo ni sawa na Sh300,000 (dola 2,865) kwa mwezi au sawa na Sh3.6 million (dola 34, 285) kwa mwaka.
Hadi kufikia wiki iliyopita, Kenya ilikuwa imeondoa kodi na makato mengine kwa askari wa Kenya kwa ajili ya kufanya kazi kwa amani ya kulinda Wakenya.
Wakati majeshi yakielekea mpakani, walipakodi wameanza kukumbana na machungu ya kodi kubwa tangu uhuru, na kwamba wataalam wa masuala ya kiuchumi wamesema itakuwa juu.
Maofisa wa Usalama hawakuwa tayari kusema kiasi gani cha fedha jeshi litatumia katika muda wa mapambano haufahamiki na pia, mapambano ya jeshi huvuruga uchumi na bajeti za nchi.
“Pesa za vita, huwezi kuziweka katika bajeti ya maendeleo. Ni kama pesa za dharura. Kama hazitoshelezi, sasa ni wakati wa serikali kuangalia, miradi gani ya kuisimamisha na fedha kuelekezwa huku,” anasema Simiyu Werunga, machambuzi wa masuala ya usalama.
Serijkali inaingia katika vita ambayo haikupangiwa bajeti huku serikali ikikabiliwa na upungufu wa Sh236 billion kati ya Sh1.2 trilioni ya fedha za bajezi kama ilivyoelezwa na  Waziri wa Fedha, Uhuru Kenyatta mapema Juni.

Majeshi ya Kenya yasonga mpakani

Vikosi vya Jeshi la Kenya vikisonga mbele. Picha ya Daily Nation.
Majeshi ya Kenya yakienda Liboi, karibu na mpaka wa Somalia tayari kwa mapambano dhidi ya makundi ya waasi wa Somalia yakiongozwa na kikundi cha Al-Shabaab.
Tayari maguruneti mawili yameshalipuka katikati ya jiji la Nairobi na watu kadhaa kujeruhiwa huku ikiripotiwa mtu mmoja kufariki dunia.

Friday, 14 October 2011

Yanga yaishinda Kagera Ligi Kuu Bara

Muuaji wa Kagera Sugar,
Kenneth Asamoah.
Mabingwa wa soka Tanzania, Yanga, wameendeleza wimbi la ushindi kwa kuilaza Kagera Sugar bao 1-0 katika mchezo kali ya Ligi Kuu kwenye Uwanja wa Taifa leo.

Yanga iliyokuwa nyuma ya hasimu wao Simba kwa pointi 10, imejivuta sana na kufikisha pointi 15 na kubakisha pointi tatu kuwafikia mahasimu wao. Simba itashuka dimbani Jumapili kucheza na African Lyon kwenye Uwanja wa Taifa.

Katika mechi hiyo, bao la Yanga lilifungwa na Kenneth Asamoah.

Ligi ya Mabingwa Ulaya wiki ijayo

Mechi za Jumanne Okt. 18 2011
CSKA Moscow v Trabzonspor, Kundi B, 17:00
Dinamo Zagreb v Ajax, Kundi D, 19:45
FC Basel v Benfica, Kundi C, 19:45
Lille v Inter Milan, Kundi B, 19:45
Man City v Villarreal, Kundi A, 19:45
Napoli v Bayern Munich, Kundi A, 19:45
Real Madrid v Lyon, Kundi D, 19:45
SC Otelul Galati v Man Utd, Kundi C, 19:45

Jumatano, Okt. 19, 2011
AC Milan v BATE Borisov, Kundi H, 19:45
Barcelona v Plzen, Kundi H, 19:45
Bayer Leverkusen v Valencia, Kundi E, 19:45
Chelsea v Genk, Kundi E, 19:45
FC Porto v Apoel Nicosia, Kundi G, 19:45
Marseille v Arsenal, Kundi F, 19:45
Olympiakos v Borussia Dortmund, Kundi F, 19:45
Shakhtar Donetsk v Zenit St Petersburg, Kundi G, 19:45

Tuesday, 11 October 2011

Egypt crowned African champions to book a World Cup berth

Egypt's coach (sec. R) with his players after crowned the tittle.

Egypt was crowned African champions following their thrilling victory over giants Cameroon 3-1 (20-25, 25-28, 25-20, 25-22) in the final of the 2011 Men’s African Nations Championship held in Tangier, Morocco on Thursday.  Egypt secured a ticket to the 2011 FIVB World Cup set to take place in Japan from November 20 to December 4.

  The African champions will now move onto the Olympic qualifying event, with the top three from there earning a berth at the London 2012 Olympic Games.

 Egypt achieved an unpreceeded record of wining the title for the fourth in row and a total of 6 crowns, but they still behind Tunisia who has eight trophies under their name and deprived Cameroon from gaining their third cup

 Meanwhile Tunisia returned back to podium after being out two years ago when they were ranked fifth as they outlasted Algeria 3-1 (28-26, 19-25, 25-18, 25-22) in the bronze medal match.

 The final was attended by Tangier Governor Hassar, CAVB President Dr Amr Elwani, Morocco Volleyball Federation President Abdelhadi Ghzali, Local organizing committee president Lahcene Chater, CAVB Vice President Majore Timba and Board members Mory Keita and Hassan Ahmed as well as a lot of the local authorities.

Final Match
Egypt Beat Cameroon 3-1 (20-25, 25-28, 25-20, 25-22)
                                                                                
 Defending champions Egypt succeeded to keep the African title on their homelands after the down the struggling Cameroon team 3-1 (20-25, 25-28, 25-20, 25-22) in a fantastic final in front of 3000 Moroccan spectators most of them supported Egypt.

 “We didn’t expect this big support from the Moroccan spectators who made us fell as if we are playing at home,” Said Egypt coach Sherif El Shemerly happily after the match.
 “I’m very happy to achieve my first title with the senior national team after a lot of achievements with the youth and Junior teams and now we are looking forwards to represent Africa in the World Cup. I’m happy with the performance of all my players because most of them apply our a strategy against a strong team like Cameroon.” He added.

 Cameroon started the match as the better side when they used the spikes of Jean Ndaki from position 2 and Didier Sali in position 4 to lead 8-5 at the first TTO. Egytp team made a lot of reception and service mistakes that allowed Cameroon to stay ahead 16-12 in the first technical timeout. Although Egypt struggled to come back through the well known spike service of Ahmed Salah and Abdalla Abdel Salam, but Cameroon palyers became highly motivated to win the set and they made it 25-20.
 Egypt started the second set with organized line up and succeeded to come back 4-1 for Cameroon to lead for the first time 8-7 at the first TTO. Cameroon came back through the quick attacks of Zamgum Nongny and Sem Dolegombai to lead narrowly 16-15 at the second TTO. Mohamed Abdel Moneim and Saleh Fathy started working from position 4 with the combinations of their skilful setter Abdalla to win the set 25-18 after a group of mistakes form Cameroon team in spiking and receiving.
 Egypt continued their dominance through the service in the third set while Cameroon coach started to make some substitutions that disturb the unity of the team and Egypt succeeded to use this to win the set 25-20 after three aces from Salah.
 Cameroon emerged back in the fourth set to save the match and their big gun Ndaki hammered the Egyptians with his attacks to lead 8-7. The Egyptian team used the strategy of the quick attacks through the centers Abdel Latif Osman and Rashad Shebl to win the difficult set 25-22.  

Bronze Medal Match
Tunisia beat Algeria 3-1 (28-26, 19-25, 25-18, 25-22)
                                                      
 Tunisia won the critical points of each set in their way to see off Algeria 3-1 (28-26, 19-25, 25-18, 25-22) in the bronze medal encounter lasting 98 minutes. Tunisia achieved the bronze medal for the
 The match started with a tight competition between both teams with Algeria having the upper hand after leading 8-7 at the first TTO. The match went point by point with both teams deploying their block against the main attackers. Algeria opposite attacker Taoufik Mahdjoubi was prominent in his powerful attacks while his Tunisian counterpart Hichem Kaabi did a good job in his skilful attacks that made his team stay in draw till 20-20. Algeria led again 24-23 with Billel Soualem spikes, but Tunisia saved two set points before Tunisia won 28-26.
 The second set showed Algerian dominance through their better reception and they led 8-5 at the first TTO. The Tunisian team tried to come back through their experienced spiker Nooreddine Hfaied and Hamza Nagga, but Algeria again arranged their combinations using Mahdjoubi and Soualem to lead 16-11 at the second TTO before they continued their wide lead till they won the set 25-19 to draw 1-1.
 The third set again started competitive till the draw 5-5 when Tunisia emerged with the spikes of Kaabi and Ismail Moalla to lead 16-11 at the second TTO. Tunisia led the situation with their good reception to win the set 25-18.
 Algeria struggled to save the match as the coach made some substitutions fielding back the captain Ali Kerboua, but Tunisia were more motivated to win as they used the spike service of Nagga and Moalla to win several popints beside the fast attacks through the centers to win the set 25-22 and the match 3-1.

Individual Awards
  • Best Setter: Abdalla Abdel Salam (EGY)
  • Beast Libero: Rafik Djoudi (ALG)
  • Best Digger: Anwer Taouerghi (TUN)
  • Best Blocker: Sem Dolegombi (CMR)
  • Best Server: Ahmed Salah (EGY)
  • Best Spiker: Jean Ndaki (CMR)
  • Most Valuable Player MVP: Ahmed Salah (EGY)

Final Results

Final:
Cameroon v Egypt (20-25, 25-28, 25-20, 25-22) 
Bronze medal:
Tunisia v Algeria 3-1 (28-26, 19-25, 25-18, 25-22)
5-6 places:
Congo Brazzaville v Morocco 3-1 (25-23, 25-22, 18-25, 25-21)
7-8 places:
South Africa v Botswana 3-1 (25-23, 25-22, 21-25, 26-24)

 All Results and Ranking
Final ranking
  1. Egypt
  2. Cameroon
  3. Tunisia
  4. Algeria
  5. Congo Brazzaville
  6. Morocco
  7. South Africa
  8. Botswana

 

Kikapu kinaposhika kasi Indoor

Kantore Sandra (kushoto) wa timu ya kikapu ya Berco Stars ya Burundi  akijaribu kufunga huku 
Lucy Augustino wa Jeshi Stars akimtazama wakati wa Mashindano ya Klabu
Bingwa ya Kikapu Kanda ya Tano Afrika yanayoendelea kwenye Uwanja wa Ndani wa Taifa jijini
Dar es Salaam. Picha ya Odoyo Jackson wa Mwananchi.

Chamudata ilivyomuunga mkono Msama


Mlezi wa Chama cha Wanamuziki wa Nyimbo za Injili, Martha Mlata
(kushoto) ambaye
pia Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Singida, akimkabidhi tuzo
Mkurugenzi wa Msama Promotions.

* Taasisi nyingine nazo zimuunge mkono
* Asomesha yatima 50, asaidia wajane 25
* Adhamiria kutoa vitanda hospitali Mtwara
* Sasa anamsubiri Lukuvi kumtafutia wafadhili

Mwandishi Maalum
"NINACHOWEZA kusema ni kwamba Kampuni ya Msama Promotions imedhamiria kutekeleza kwa vitendo jukumu kubwa la Serikali ya Awamu ya Nne ya Rais Jakaya Kikwete la kupambana na ukosefu wa ajira, na tuko mstari wa mbele kuwasaidia watoto yatima."
Hiyo ni kauli ya Mkurugenzi Mtendaji wa Msama Promotions, Alex Msama anayebainisha kwamba kutokana na dhamira hiyo, ndiyo maana wamekuwa mstari wa mbele kuandaa matamasha ya muziki wa Injili, lengo likiwa ni kupata fedha kuchangia watoto yatima.
Kutokana na kuwa mstari wa mbele kudhibiti kazi za wasanii, Chama cha Wanamuziki wa Injili Tanzania (Chamuta) kimeamua kumpa tuzo Msama. Heko Chamuta kwa kuthamani mchango wake, na kutoa changamoto kwa taasisi nyingine kuiga mfano huo.
Chamuta wakiongozwa na Mbunge wa Viti Maalumu, Martha Mlata waliandaa tafrija maalumu kwa ajili ya kumpongeza Msama kwa kutambua mchnago wake huku wakimkabidhi tuzo, ikiwa ni sehemu ya kutimiza wajibu wao kama wadau.
Msama amekuwa akitumia muda wake mwingi kupambana na maharamia wanarudufu kazi za wasanii, na kutokana na tuzo aliyopewa, anasema ndio kwanza mapambano yameanza, kwani ameahidi kuongeza kasi zaidi akishirikiana na Jeshi la Polisi nchini na taasisi nyingine husika.
Mlata alitumia fursa hiyo kuiomba Serikali kuunga mkono jitihada za Msama, ikiwa ni pamoja na Watanzania wengine kwa ujumla.
Akizungumzia mambo mengine zaidi, Msama anasema mapato yanayotokana na matamasha mbalimbali ikiwa ni pamoja na la Pasaka kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee, Dar es Salaam, kiasi yalitumika kuchangia wajane 25 wasiojiweza na kusomesha watoto yatima katika mikoa ya Dodoma, Tabora na Shinyanga.
Msama anasema huo ndio utaratibu wao, fedha wanazopata wamekuwa wakitumia kusomesha yatima na kuwatafutia ajira mbalimbali wasiojiweza ikiwa ni pamoja na wengine kupata mafunzo ya kunadi vitu kupitia kampuni yake ya Msama Auction Mart.
Mkurugenzi huyo anasema mpaka sasa wanasomesha wanafunzi takriban 50 katika shule mbalimbali Dar es Salaam zikiwamo St. Mary's, George Washington, VETA, Lugalo, Colnelius na Biafra.
Anasema pia wamekuwa wakitoa semina za kusaidia wajane, yatima na vijana wasio na ajira ikiwa ni pamoja na kuwapa mbinu za kufanya biashara na kuachana na dawa za kulevya.
Msama Promotions pia ilikamilisha ahadi yake ya kuwasaidia wanawake wajane fedha za mitaji ya biashara kwa kuwakabidhi wajane 25 fedha taslimu sh. 150,000 kila mmoja, jumla ikiwa ni sh. milioni 4.
Msama anasema alitimiza ahadi aliyoitoa wakati wa maandalizi ya tamasha la Pasaka lililofanyika Aprili 24 mwaka huu katika ukumbi wa Diamond Jubilee huku mgeni rasmi akiwa Rais Kikwete.
Msama anasema fedha hizo zilipatikana kutokana na mauzo ya albamu ya Haleluya Collection Vol 5 iliyozinduliwa katika tamasha la Pasaka.
Wanawake hao wajane waliokabidhiwa fedha hizo za mitaji wametoka mikoa ya Dar es Salaam, Pwani na Morogoro. Pia fedha zilizopatikana kwenye tamasha hilo zinatumika kusaidia kuwasomesha watoto yatima mikoa ya Tabora, Dodoma na Shinyanga kwa awamu hii.
Msama Promotions tayari imeshatoa msaada wa sh. milioni 3 kwa waathirika wa mabomu yaliyotokea kwenye kambi ya jeshi Gongo la Mboto, Dar es Salaam.
Vitu vilivyotolewa ni magunia manne ya mchele, kila moja likiwa na kilo 120, magunia mawili ya maharage, magunia 10 ya unga wa mahindi, mifuko miwili ya sukari, mifuko mitatu ya unga wa ngano yenye kilo 25 kila moja na ndoo mbili za mafuta ya kupikia.
"Lengo kubwa la tamasha la Pasaka linaloratibiwa na Msama Promotions ni kusaidia watoto yatima na jamii kwa ujumla... ndio maana hata  walioathirika kwa kwa mabomu tuliwasaidia," anasema Msama.
Akipokea msaada huo, mtangazaji wa Clouds FM, Anthonio Nugazi anayeendesha kipindi cha Kambi Popote, alimshukuru Msama kwa kuonesha moyo wa kujitolea, na akatoa mwito kwa Watanzania wengine kuiga mfano.
Tamasha la Pasaka la nyimbo za Injili za kumsifu Mungu, lilifanyika kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee, Dar es Salaam, Apili 24 mwaka huu, Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma na Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza na kushirikisha wasanii kutoka nchi za Kenya, Zambia na Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo.
Akisoma risala mbele ya Rais Kikwete kuhusu tamasha hilo ambalo mwaka huu liliadhimisha jubilee ya miaka 10 tangu kuanzishwa, Askofu wa Kanisa la TAG, Lawrence Kameta alimuomba Rais Kikwete kuwashauri viongozi wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) kupunguza gharama za vibali vya kuwaalika wasanii wa nje kwa ajili ya tamasha hilo.
Alisema kwa vile tamasha hilo limelenga kusaidia watu wasiojiweza, wajane na walemavu na kwamba si tamasha la kibiashara, ipo haja ya BASATA kupunguza gharama hizo ili miaka ijayo liwe na waimbaji wengi kutoka nje ya nchi ikiwa ni moja ya njia ya kudumisha umoja kati ya Tanzania na nchi jirani.
Ombi jingine lililotolewa na kampuni hiyo kwa Rais Kikwete ni kupewa eneo la ardhi itakayojengwa ili makundi ya watu wasiojiweza wakutane katika eneo hilo na kupata msaada wa mahitaji yao.
Pia waliomba Serikali kusaidia kushawishi kampuni za vinywaji baridi na za simu kuunga mkono kufadhili tamasha hilo kwani hufikia kubaki na madeni baada ya tamasha kumalizika.
Akijibu ombi hilo, Rais Kikwete aliwaeleza BASATA kutekeleza ombi hilo kwani kazi inayofanywa na Msama Promotions ya kusaidia makundi ya watu wasiojiweza ni kubwa na linapojitokeza tatizo la kuhitaji msaada wa kulifanikisha, Serikali inatakiwa kuonesha msaada wake.
Kazi ya kutafuta wafadhili na kuchangisha, Rais Kikwete alimkabidhi Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Uratibu, Sera na Bunge, William Lukuvi kwa vile anaimudu.
Wasanii wa nyimbo za injili wakiimba wimbo maalumu wa
 kutimiza miaka 50 ya Uhuru

Friday, 30 September 2011

Dewji: Siafiki Angetile kumtetea Poulsen


Na Mwandishi Wetu
MFANYABIASHARA na mwanamichezo maarufu nchini, Azim Dewji amesema kuwa, kamwe haafikiani na utetezi unaotolewa na Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Angetileh Osiah anayedai Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Jan Poulsen hawezi kufukuzwa kwa sababu ana mkataba wa miaka miwili.

Dewji aliyewahi kuifadhili Simba na kuipa mafanikio makubwa Afrika, alisema jana jijini Dar es Salaam kuwa, wadau wana nafasi kubwa katika ustawi wa soka ya Tanzania, hivyo wasipuuzwe kwa majibu ya juu juu.

Alisema: “Nimesoma taarifa inayomnukuu Katibu Mkuu wa TFF kwamba Paulsen hawezi kutimuliwa kwa sababu ana mkataba wa miaka miwili, tena kwa sababu ya maoni ya wadau.

“Binafsi nasema hii si sahihi. Kocha anapimwa kwa vigezo vingi, lakini kama ameshindwa kazi na haoneshi dalili za kuelekea kufanikiwa, kwanini aendelee kuachwa kazini? Nahisi Angetile amepotoka na kamwe siafiki utetezi wake.”

Dewji aliongeza kuwa, kocha huyo raia wa Denmark alipaswa kuifanyia mapinduzi ya soka Stars, lakini anashangazwa kuona kila kukicha akifanya sawa na waliomtangulia, kuita kikosi kwa ajili ya mechi fulani huku akiwatumia wachezaji `wazee’ badala ya kuibua na kuelea vipaji vipya kwa ustawi wa soka katika miaka ijayo.

Angetile Osiah
“Hakuna jipya na wadau wanakata tamaa, ndiyo maana wanatoa ushauri kwa sababu wanaipenda timu yao. Wakiendelea kukatishwa tamaa, nani atakwenda uwanjani na TFF itapata wapi fedha? Ni vyema wakalitafakari hili, kwani tunashuhudua makocha wenye mikataba wakiachishwa kazi baada ya kushindwa kukata kiu ya waajiri wao,” alisema Dewji.

Osiah, jana alikaririwa na vyombo vya habari akimtetea Poulsen baada ya wadau mbalimbali wa michezo nchini kuhoji uhalali wa kocha huyo kuendelea kutafuta fedha za Watanzania, ilhali haoneshi mwelekeo wowote, zaidi ya kuporomosha kiwango cha wachezaji wa Taifa Stars.

Miongoni mwa wadau hao ni Mbunge wa Kilwa Kaskazini, Murtaza Mangungu aliyeonesha hofu ya Tanzania kutonufaika na lolote kutoka kwa kocha Poulsen.

Akizungumza na waandishi wa habari za michezo juzi, Osiah alisema: “Tunaheshimu maoni ya wadau wetu, akiwamo Mbunge Mangungu (Murtaza), ila lazima tuelewe kuwa Poulsen yupo kisheria na mkataba wake ni wa miaka miwili, hivyo hatuwezi kumuacha kwa mtindo wanaoutaka wao.

Poulsen aliyetua nchini kuirithi mikoba ya Mbrazil Marcio Maximo mwaka 2010, hajapata mafanikio makubwa akiwa na kikosi cha Stars, ukiondoa `ngekewa’ ya kutwaa Kombe la Challenge, ikiwa ni kwa mara ya kwanza tangu mwaka 1994. Ilishindwa kwa `matuta’ kuanzia hatua ya makundi hadi fainali.

Na hata baada ya kuingia katika michuano ya awali ya Kombe la Mataifa ya Afrika kwa mwaka 2012 na ile ya Kombe la Dunia mwaka 2014, Stars imeendelea kuwa ile ile ya kubahatisha uwanjani, hali inayompa wakati mgumu Poulsen aliyewabwaga wenzake watano katika mchujo wa mwisho wa kundi la makocha 59 waliokuwa wameomba kumrithi Maximo.


Thursday, 29 September 2011

Matokeo Ligi ya Mabingwa Ulaya mechi zilizochezwa jana usiku

Arsenal wakishangilia bao....
Kundi E
Valencia 1 Chelsea 1
Bayer Leverkusen 2 Racing Genk 0

Kundi F
Olympique Marseille 3 Borussia Dortmund 0
Arsenal 2 Olympiakos Piraeus 1

Kundi G
Shakhtar Donetsk 1 APOEL Nicosia 1
Zenit St Petersburg 3 Porto 1

Kundi H
AC Milan 2 Viktoria Plzen 0
BATE Borisov 0 Barcelona 5

Wednesday, 28 September 2011

...Mashabiki wa Michael Jackson

Mashabiki wa Michael Jackson nje ya mahakama...
Kaka wa Michael Jackson, Jermaine...

Wanandugu wa Michael Jackson wakienda mahakamani kusikiliza kesi ya daktari wa MJ

Wazazi wa Michael Jackson...
Janet Jackson naye akiingia mahakamani..

Mancini amtimua Tevez Man. City

Carlos Tevez akiitumikia klabu yake.
LONDON, England
Kocha wa Manchester City, Roberto Mancini amesema anataka kuona Carlos Tevez "anajiondoa mwenyewe klabuni" baada ya kugoma kuingia katika mechi ya Ligi ya Mabingwa dhidi ya Bayern Munich.
Mancini alimtaka mchezaji huyo kuingia dakika 35 wakati timu yake ilipokuwa nyuma kwa mabao 2-0.
Mancini alisema: "Kama mimi ni kocha hapa, sitaki kumuona. Ameshamalizana na mimi.
"Kama tunataka kuimarisha timu, kwa mtu kama Carlos hatufai. Kwangu tumemalizana."

Man. United chupuchupu, Real yaua

LONDON, EnglandManchester United ilinusurika kuumbuka kwenye Uwanja wake wa Old Trafford baada ya kupata bao dakika ya 90 lililofungwa kwa kichwa na Ashley Young na kufanya matokeo kuwa 3-3 dhidi ya Basel katika mechi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya Kundi C. Mabingwa hao wa Uswisi waliokuwa nyuma kwa mabao 2-0 walisawazisha na kufunga lingine na kufanya matokeo kusomeka 3-2.
United walionekana kuridhika na mabao mawili ya kipindi cha kwanza ya Danny Welbeck, lakini Basel ilisawazisha kabla ya Fabian Frei kufunga la tatu baada ya mabao ya Alexander Frei.
Wakati ndugu zao wakisalimika, Manchester City walitandikwa mabao 2-0 na Bayern Munich huku Mario Gomez akifunga mabao yote mawili katika mechi hiyo ya Kundi A na kuifanya Bayern kuwa na pointi sita katika mechi mbili.
Real Madrid, kwa upande wake, ilikuwa ikisaka rekodi ya taji la 10 la Ulaya kwa kujipatia pointi sita katika mechi ya Kundi D baada ya kuizabua 3-0  Ajax Amsterdam kwa mabao ya Cristiano Ronaldo, Kaka na Karim Benzema.
Inter Milan iliyokuwa nyuma kwa mabao 2-0 mbele ya CSKA Moscow iliibuka na kushinda mabao 3-2 baada ya kazi nzuri ya Mauro Zarate aliyefunga bao la ushindi na kufanya kikosi cha kocha, Claudio Ranieri kuendelea kujipa matumaini ya kufanya vizuri.
Mechi nyingine, Napoli iliifunga Villarreal 2-0 mechi ya Kundi A, Trabzonspor ikatoka sare ya 1-1 na Lille ikiwa ni mechi ya Kundi B wakati Benfica iliifunga Otelul Galati 1-0 katika Kundi C. Nayo Olympique Lyon ikailaza Dinamo Zagreb 2-0 katika mpambano wa Kundi D.

Mechi za Makundi E-H zinazochezwa leo Jumatano Sept. 28, 2011

Zenit St Petersburg v FC Porto
AC Milan  v Plzen
Arsenal  v Olympiakos
BATE Borisov v Barcelona
Bayer Leverkusen v Genk
Marseille  v Borussia Dortmund
Shakhtar Donetsk v Apoel Nicosia
Valencia  v Chelsea

Tuesday, 27 September 2011

Jackson's doctor Murray goes on trial

Michael Jackson's personal physician, Conrad Murray, has gone on trial in Los Angeles, charged with involuntary manslaughter of the singer.
Prosecutors say he acted with "gross negligence" and gave Jackson a lethal dose of the sedative propofol, on the night he died in June 2009.
The defence says Jackson gave himself too much of the drug, a sleeping aid.
If convicted, Dr Murray, 58, could face four years in jail and the loss of his medical licence.
Slurred recording
In Tuesday's opening statement, lead prosecutor David Walgren told the court the evidence would show "Conrad Murray repeatedly acted with gross negligence, repeatedly denied appropriate care to his patient, Michael Jackson".
Lead prosecutor, David Walgren, plays an audio recording said to be from Dr Conrad Murray's mobile phone
"That misplaced trust... cost Michael Jackson his life."
The court heard a recording of Jackson slurring while talking about planned comeback concerts.
Mr Walgren said the audio, aired in public for the first time, had come from Dr Murray's mobile phone.
"When people leave my show, I want them to say, 'I've never seen nothing like this in my life'," says the voice on the audio.
The prosecutor said Jackson's difficulty in speaking on the recording showed that Dr Murray ought to have realised the star should not have taken any more propofol.
Mr Walgren said that after administering a dose of the drug on the date of Jackson's death, Dr Murray had not been attentive to the star's health.
'Abandoned'
The prosecutor said the doctor had left to go to the bathroom and checked his mobile phone.
 
Chief prosecutor David Walgren: Michael Jackson trusted his life to the medical skills of Conrad Murray
"He [Murray] left him [Jackson] there, abandoned him to fend for himself," the prosecutor said.
Mr Walgren said when Dr Murray found Jackson unconscious, he did not immediately call the emergency services, instead telling a bodyguard to do so 20 minutes later.
Dr Murray also did not mention to paramedics or emergency room doctors that he had administered propofol, according to the prosecutor.
Hundreds of Jackson fans gathered outside court as the trial began with opening statements from defence and prosecution. The proceedings are being televised and broadcast online.
Jackson choreographer Kenny Ortega was set to be the first prosecution witnesses to take the stand.
Mr Ortega was expected to lead the court through some footage from Jackson's final rehearsals as the 50-year-old star prepared for his series of comeback concerts.
That video eventually became part of a documentary, This Is It, directed by Mr Ortega.
A judge has blocked some details of Jackson and Dr Murray's lives being discussed at the trial.
Extra dose?
Jackson's history with drugs and financial troubles, as well as Dr Murray's debts and personal affairs, will not come out in court.
Both sides were expected to focus on Jackson's last hours.
Multiple witnesses, including security guards, paramedics and emergency room doctors are to be called.
The prosecution also plans to play a recording of Dr Murray's police interview two days after Jackson's death, in which the doctor says he gave the singer propofol for his insomnia.
The disclosure led to charges being brought against Dr Murray in February 2010.
Propofol is usually administered intravenously, often during surgery.
Medical experts are expected to testify about the sedative's effects, as well as how a trace amount of the drug was found in Jackson's stomach.
Defence lawyers are putting forward the theory that Jackson drank or somehow administered an extra dose of propofol after Dr Murray left.
The trial is expected to last about five weeks.
The jury comprises seven men and five women, one African American, six whites and five Latinos.
BBC News

R.I.P. Wangari Maathai

President Barack Obama (Left) and his wife Michelle (Right) and Prof Wangari Maathai (Centre) during an AIDS awareness campaign in Nairobi, Kenya, in 2006. Photo by DailyNation.

Poulsen aita 23 kuikabili Morocco

Dua kabla ya mchezo



Release No. 98

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Septemba 27, 2011
 Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Jan Poulsen leo ametangaza kikosi cha wachezaji 23 kwa ajili ya mechi ya mwisho ya mchujo kuwania tiketi ya kucheza fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika mwakani dhidi ya Morocco.
Kikosi hicho kitaingia kambini Septemba 29 mwaka huu jijini Dar es Salaam, na kinatarajiwa kuondoka nchini Oktoba 6 mwaka huu kwenda Casablanca, Morocco kwa ajili ya mechi hiyo itakayochezwa Oktoba 9 mwaka huu kwenye mji wa Marrakech.
 Wachezaji walioitwa ni makipa Shabani Dihile (JKT Ruvu Stars), Juma Kaseja (Simba) na Shabani Kado (Yanga). Mabeki wa pembeni ni nahodha Shadrack Nsajigwa (Yanga), Erasto Nyoni (Azam), Idrissa Rajab (Sofapaka, Kenya) na Amir Maftah (Simba). Mabeki wa kati ni Aggrey Morris (Azam), Juma Nyoso (Simba) na Victor Costa (Simba).
 Viungo wakabaji ni Henry Joseph (Kongsvinger IL, Norway), Nurdin Bakari (Yanga), Shabani Nditi (Mtibwa Sugar) na Jabir Aziz (Azam). Viungo washambuliaji ni Nizar Khalfan (Vancouver Whitecaps, Canada), Mrisho Ngassa (Azam) na Ramadhan Chombo (Azam).
 Washambuliaji ni Abdi Kassim (DT Long An, Vietnam), Mbwana Samata (TP Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo- DRC), Dan Mrwanda (DT Long An, Vietnam), Athuman Machupa (Vasalund IF, Sweden), John Bocco (Azam) na Hussein Javu (Mtibwa Sugar).    
Boniface Wambura Mgoyo
Ofisa Habari - TFF

 

Dr Murray faces jury over Jacko death

LOS ANGELES, USA
More than two years after Michael Jackson's sudden death, the singer's personal physician is to stand trial on Tuesday. Dr Conrad Murray, 58, has pleaded not guilty to a charge of involuntary manslaughter. If convicted, the maximum sentence is four years in prison.
It was a hot midsummer day in Los Angeles on 25 June, 2009. Hollywood was mourning the loss of the actress Farrah Fawcett, as fans and celebrities paid tribute to the TV star, who had died from cancer, aged 62.
But that day will be remembered for another, altogether unexpected death and for the extraordinary outpouring of grief it provoked.
Pop star Michael Jackson, a month shy of his 51st birthday, was rushed to hospital and pronounced dead, his brother Jermaine confirming the news to stunned fans in a hastily-arranged press conference.
Jackson had recently stepped back into the limelight. He was rehearsing at the Staples Centre arena in Los Angeles for This Is It, his hugely anticipated concert series, which was due to start at the O2 in London on 13 July.
The night before his death, he worked until after midnight. The next day, shortly after noon, he was discovered unconscious in his bedroom by his physician Dr Conrad Murray.Dr Conrad Murray faces up to four years in prison if convicted
What happened in the time between those two events remains a mystery.
At a preliminary hearing, several witnesses gave detailed accounts of the frenzied activity at Jackson's home after the singer was found to be unresponsive.
The singer's death, according to the Los Angeles County Coroner, was a homicide caused by "acute Propofol intoxication." Propofol is a sedative that is normally used in hospitals to induce or maintain anaesthesia during surgical procedures.
But it will be up to a jury to decide whether the actions of Dr Murray, during the frantic efforts to revive the singer and in the hours before, caused his death.
BBC News

Persie aendelea kuiwekea 'pozi' Arsenal


Robie van Persie (katikati) wa Arsenal akiwa chini ya ulinzi wa wachezaji wa Newcastle katika moja ya mechi za Ligi Kuu ya England. Persie ameendelea kuidengulia Arsenal baada ya kukaririwa leo akisema hajaamua kama ataitumikia klabu hiyo ya Emirates kwa muda mrefu.


Vumbi Ligi ya Mabingwa Ulaya leo

C. Ronaldo, Real Madrid
Ligi ya Mabingwa Ulaya, inaingia hatua nyingine leo, baada ya timu kadhaa kufanya vema katika mechi za ufunguzi.
Manchester United, Manchester City na Inter Milan zina kazi ngumu leo kujihakikishia nafasi ya kusonga mbele.
Kila mmoja anatambua kuwa hakuna timu iliyotwaa ubingwa mara mbili tangu kuanzishwa kwake miaka 20 iliyopita, kila mmoja anaangalia jinsi gani ya kuivua ubingwa Barcelona.
Klabu hiyo ya Catalan itataka kujiimarisha zaidi kwani yenyewe na United zilitoka sare. Man United ilitoka sare na Benfica, City ilifanya hivyo kwa Napoli lakini Inter ilishangaza wengi kwa kuchapwa na Trabzonspor ikiwa nyumbani.
City, na United ambazo ziko kileleni mwa Ligi Kuu ya England, ilicheza na Napoli, na kuwalazimisha sare ya 1-1 kwenye Uwanja wa Etihad na kumwacha kocha, Roberto Mancini akijisifu "Nilichanganyikiwa kwa sababu ilikuwa mechi ya kwanza".
Mechi za leo
Bayern itakuwa na kazi ya kupunguza makali ya washambuliaji wa City wanaojengwa na Tevez, Balotelli, Owen Hargreaves na Yaya Toure.

W. Rooney, Man United

Hata hivyo, Bayern inajivunia ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Villarreal na ushindi wake leo utaisaidia kujiweka katika nafasi nzuri zaidi.
Nayo Manchester United, kwa upande wake itakuwa na kibarua cha vijana wa Uswisi; Basel lakini watamkosa, Wayne Rooney.
Kocha wa United; Sir Alex Ferguson ameanza kuingia hofu kukosekana kwa Rooney, huku akiendelea kusikilizia maumivu ya Javier Hernandez aliyeumia katika mechi waliyotoka sare ya 1-1 na Stoke.
Naye kocha wa Basel, Thorsten Fink anasema ana kila sababu ya kuisimamisha United, kama alivyofanya kwa Bayern Munich ilipofungwa 1999 na Red Devils mechi ya Barcelona.
Inter ambayo ilianza vibaya ligi hiyo na baada ya kumtimua kocha wake, Giun Piero Gasperini na wamemnasa kocha wa zamani wa Chelsea na Juventus, Claudio Ranieri.
Ranieri alishinda mechi ya kwanza 3-1 dhidi ya Bologna Jumamosi, lakini Wesley Sneijder, beki wa Brazil, Maicon na  kiungo wa Serbia, Dejan Stankovic watakosa mechi ya Kundi B, itakutana na CSKA mjini Moscow.
Katika kundi hilo, mabingwa wa Ufaransa, Lille itakutana na Trabzonspor wakati Lyon itacheza na Dinamo Zagreb, na Real Madrid itakuwa nyumbani kuivaa Ajax.

Adebayor: Nilicheza jicho moja sioni

Adebayor kushoto. PHOTO/Getty.
LONDON, England
Mshambuliaji wa zamani wa Arsenal, ambaye aliingia kipindi cha pili katika mechi dhidi ya Wigan alicheza huku akiwa haoni jicho moja baadaya kugongana na mchezaji wa upinzani, lakini akasema anataka kuwa fiti ili aweze kufunga bao la kwanza dhidi ya Arsenal kufuta bao lile alilolaumiwa kwa kushangilia sana dhidi ya Arsenal alipokuwa akiitumikia Manchester City miaka miwili iliyopita."Sikuwa nauona mpira. Sikuwa naona mtu anayekuja," anasema Adebayor, ambaye hata hivyo, alicheza mechi hiyo hadi mwisho. "Lakini nzuri zaidi, nilikuwa na jicho moja, lakini tuliondoka na pointi tatu.Kipindi cha kwanza nilicheza vizuri kwa sababu nilikuwa naona kwa macho yote."

Keyshia, Gibson kufunga ndoa ya kufuru

HAWAII, Marekani
NYOTA wa R&B, Keyshia Cole amerudia kuzungumzia mipango ya sherehe za harusi yake itakayofanyika kwenye kitongoji cha Hawaii. Aliyasema hayo katika kipindi chake; TV show.
Keyshia, 29, anasema....nilikuwa na nyota wa kikapu wa Cleveland Cavaliers, Daniel Gibson wikiend na akaniambia maneno matamu baada ya kugombana miezi minne iliyopita.
Nyota huyo aliwaambia pia mashabiki wake, "Anataka tufunge ndoa ya 'kufuru' na anaandaa utaratibu wa kuleta wazazi wake hapa. Amenipa kitu 'baab kubwa' siwezi kusahau...ananipenda! Nimefurahi sana!"
Sherehe za harusi hiyo zitaonyeshwa moja kwa moja kupitia kipindi cha Cole's reality TV show cha Family First, kinachoanza mapema February.
Mwanamuziki huyo kwa sasa ana watoto wawili, Daniel, mwenye miezi (10), na Gibson. Wawili hao walioana katika hafla ndogo iliyofanyika Cleveland, Ohio mapema Mei 11.

Monday, 26 September 2011

Berbatov could make a European return for Man. United

Berbatov
LONDON, England
IT is almost three years since his last Champions League goal and his mantle as fourth-choice striker is under threat from Michael Owen, yet Sir Alex Ferguson has denied he needs to repair Dimitar Berbatov's confidence ahead of Manchester United's encounter with Basel.
Berbatov has been frequently overlooked on the big occasions by Ferguson, notably the Champions League final defeat to Barcelona at Wembley in May, and may be required for United's opening home game in Europe this season. Wayne Rooney is a confirmed absentee with a hamstring injury, a problem with potential repercussions for England's Euro 2012 qualifier in Montenegro on Friday week, so too Javier Hernández with a dead leg he sustained at Stoke City on Saturday. With Danny Welbeck also easing his way back from a hamstring tear it would represent another slight on the £30.75m striker not to be selected ahead of or alongside Owen, Federico Macheda or Mame Biram Diouf.
The 30-year-old has started United's last two matches, the draw at the Britannia Stadium and the Carling Cup win at Leeds United, and perhaps that explained Ferguson's irritation when pressed on Berbatov's contribution to the Champions League campaign. "Of course he's got a part to play. He's one of our squad members and they've all got a part to play," the United manager said. "There are a lot of games in the Premier League, Champions League, FA Cup and Carling Cup. It's an exhausting season unless you use your squad."
The Guardian

'Mapro' 20 Morocco kuivaa Taifa Stars

RABAT, Morocco
Marouane Chamakh
KOCHA wa Morocco, Eric Gerets ametangaza kikosi cha wachezaji zaidi ya 20 wanaocheza soka ya kulipwa kona mbalimbali za dunia kwa ajili ya pambano dhidi ya timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars litakalofanyika Oktoba 9 kwenye mji wa Marrakech, Morocco.

Wachezaji walioitwa ni Ismail Aissati (Ajax, Uholanzi), Ahmed Ajedou (Wydad Casablanca), Jamal Alioui (Al Kharityath, Qatar), Nordin Amrabat (Kayserispor. Uturuki), Ossama Assaidi (Heerenveen, Uholanzi), Aissam Badda (FUS Rabat) na Micahael Basser wa Buraspor ya Uturuki.

Wengine ni Younes Belhanda (Montpellier, Ufaransa), Mohamed Berrabeh (Wydad Casablanca), Mbark Boussoufa (Anzhi Makhachkala, Russia), Rachid Bourabia (Mons, Belgium), Kamal Chafni (Auxerre, Ufaransa) na Marouane Chamakh wa Arsenal ya England.

Pia wamo Mohammed Chihani (Al Arabi, Qatar), Adil Chihi (Cologne, Ujerumani), Nabil Dirar (Club Brugge, Ubelgiji), Larim El Ahmadi Aroussi (Feyenoord, Uholanzi), Youssef El Arabi (Al Hilal, Saudi Arabia), Mounir El Hamdaoui (Ajax, Uholanzi) na Mostapha El Kabir wa Cagliari ya Italia.

Wachezaji wengine ni Badr El Kaddouri (Celtic, Scotland), Abdelhamid El Kaoutari (Montpellier, Ufaransa) Ayoub El Khaliqi (Wydad Casablanca), Mehdi El Moutaqui (Udinese, Italia) Youssouf Hadji (Rennes, Ufaransa) na Houssine Kharja wa Fiorentina ya Italia.

Wengine waliotajwa ni Oussama Laghrib (FUS Rabat), Nadir Lamyaghri (Wydad Casablanca), Ahmed Mohamadina (Olympic Khouribga), Mustapha Mrani (MAS), Youssef Rabeh (Wydad Casablanca), Fatah Said (Wydad Casablanca), Rachid Soulaimani (Raja Casablanca) na Adel Taarabt wa Queen Park Rangers ya England.